MTOTO WA KIGOGO AMPIGA RISASI YA KICHWA MFANYAKAZI WA BAR, AKAMATWA NA KUCHIWA GHAFLA NA JESHI LA POLISI
MTOTO WA KIGOGO AMPIGA RISASI YA KICHWA MFANYAKAZI WA BAR, AKAMATWA NA KUCHIWA GHAFLA NA JESHI LA POLISI 11:03 PM JULIUSJOSEPH.BLOGGER.COM Jeshi la polisi mkoani Arusha limemshikilia na kisha kumwachia “chapchap” mtoto wa mwenyekiti wa CCM wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro na mfanyabiashara maarufu nchini,Oscar Themi kwa kosa la kumpiga risasi ya kichwa mhudumu wa bar ya Empire iliyopo eneo la Shoprite jijini Arusha. Mtuhumiwa huyo ,Dereck Themi alishikiliwa na polisi mwishoni mwa wiki iliyopita mara baada ya kutofautiana na mhudumu huyo wakati alipompatia bili ya vinywaji aliyokuwa akitumia ndani ya bar hiyo kabla ya kumtandika risasi. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa mnamo novemba 29 mwaka huu majira ya saa 7.30 usiku mtoto huyo wa kigogo alimfyatulia risasi mhudumu huyo aliyetambulika kwa jina la Witness Erasto wakati alipompatia bili ya vinywaji. Mashuhuda...