Ukiwa na tabia hizi,mwanaume lazima akukimbie!
Ukiwa na tabia hizi,mwanaume lazima akukimbie! MUNGU ni mwema wapenzi wasomaji wa safu hii. Wikiendi nyingine tena tunakutana na kuweza kupeana darasa la uhusiano. Kujifunza ni muhimu, hakika ukifuatilia makala haya ya leo, utajifunza kitu. Twende pamoja! Kupitia safu hii nimekuwa nikipata malalamiko mengi kutoka kwa wanawake. Kilio chao kikubwa ni kukimbiwa na wanaume au kuachwa. Leo anakuwa na mwanaume huyu, baada ya muda mfupi kunatokea chokochoko, mwanaume anatimka zake. Jamaa anamkimbia na kwenda kuanzisha uhusiano mwingine. Baada ya kukimbiwa, mwanamke hakati tamaa. Anaanzisha uhusiano mwingine, ndani ya muda mfupi tu, anaambulia maumivu tena. Anabaki kujilaumu. Hajui chanzo cha yeye kukimbiwa. Matokeo ya hili, mwanamke anapoteza uelekeo. Kila mwanaume anayekutana naye anamkimbia. Mwisho wa siku anajikuta umri umeenda. Kuolewa inakuwa ni ndoto. Anaanza kulazimisha kusaka mtoto ili angalau na yeye aitwe mama. Marafiki zangu, wanaume wengi hujikuta wakiwaacha wapenz...