HAYA NAYOMATATIZO YANAYOKUMBA NDOA NA KAZI KWA KILA MWANA NDOA HILI NALO NENO...: LADY JAY DEE AOMBA TALAKA KUTOKA KWA MUME WAKE
HAYA NAYOMATATIZO YANAYOKUMBA NDOA NA KAZI KWA KILA MWANA NDOA HILI NALO NENO...: LADY JAY DEE AOMBA TALAKA KUTOKA KWA MUME WAKE Stori: Shani Ramadhan UNAWEZA ukakataa lakini ndivyo ilivyotokea, ndoa ya mtangazaji mahiri Bongo, Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteini’ na Mbongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ iliyofungwa miaka 9 iliyopita inadaiwa kuingia kidudu kufuatia mke huyo kuomba aandikiwe talaka, ni Ijumaa Wikienda pekee lenye uthubutu wa kuripoti mkasa wote. Jide akiwa na mumewe Gardner. Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, Jide au Lady Jaydee alifikia uamuzi huo baada ya Gardner kupata kazi ya kutangazia redio moja nchini Kenya. HABARI KAMILI Mnyetishaji wa kisanga hiki, aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa mara baada ya mume huyo kupata mchongo mzima alirudi nyumbani akiwa na furaha na kumwambia mkewe kuhusu bahati hiyo. “Baada ya Gardner kupata mchongo wote wa kazi alikwenda mbi...