HATIMAYE KIONGOZI MARKIA NA RAIS MPYA WA KIJIJI CHA MAISHA PLUS WAPATIKANA
Markia Mpya wa Kijiji cha Maisha Plus Elizabeth Masha kutoka Morogoro Tanzania. Rais Mpya wa Kijiji cha Maisha Plus Mary Masha kutoka Nchini Kenya Ndani ya Kijiji cha Maisha Plus/ Mama Shujaa wa chakula kila siku ya Alhamisi huwa panafanyika uchaguzi wa kumpata Rais mpya ambaye anachaguliwa na Washiriki wenyewe wa Kijiji cha Maisha Plus ambapo kati ya hao mmoja hupatikana na Marais waliopita hawapatiwi nafasi ya kugombea tena, na kwamba mama yake na Rais huteuliwa moja kwa moja kuwa Markia wa Kijiji hicho. Kazi ya uchaguzi ilianza Kijijini hapo ambapo idadi ya washiriki 36 wakiwemo vijana 16 na kinamama 20 Kila siku ya Alhamisi ni siku ya uchaguzi wa Rais wa kijiji cha Maisha Plus ambaye husimamia shughuli zote zinazofanyika katika kijji hicho. Wiki hii washiriki 10 waliteuliwa kugombea nafasi ya urais ambapo 7 ndiyo waliopigiwa kura ya siri na kupata mshindi. Washiriki wawili...