Msanii Aelezea kwa nini alikata uume wake
Je unamkumbuka mwanamuziki wa kufoka Andre Johnson ambaye alikata Uume wake mwezi Aprili na kisha kujirusha kutoka juu ya jumba moja mjini Los Angeles? Sasa basi emetoa sababu zake akisema alikuwa na akili timamu alipokuwa anafanya hivyo. Johnson, aliishangaza jamii ya wanamuziki wa kizazi kipya, kufuatia kitendo chake cha kukata uume wake Kaskazini mwa Hollywood mwezi Aprili. Madaktari walishindwa kunguanisha sehemu aliyoikata na sehemu nyeti ya mwili wake. Tangu hapo alikimya kwa miezi miwili akipokea matibabu. Lakini aliamua wiki hii kujieleza kwa nini alichukua hatua hiyo na kuambia kituo cha televisheni cha E! nchini Marekani:''Ndio nilikuwa nimetumia dawa za kulevya , lakini nilikuwa najifahamu.'' 'Mi...