TCME WASHIRIKIANA NA VETA KATIKA KUTOA MAFUNZO
TCME WASHIRIKIANA NA VETA KATIKA KUTOA MAFUNZO
Mgeni Rasmi katika sherehe za mwaka za Chama cha Wafanyabiashara
wa Madini Tanzania (Tanzania Chamber of Minerals and Energy) Katibu Mkuu
Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi akizugumza kwa niaba ya
Waziri kwa wageni waalikwa na mabalozi.(Picha na Zainul Mzige)
.Joseph Kahama aahidi ushirikiano na wachimbaji wadogo nchini
.Asema sekta ya madini kuongeza mchango wake kwenye pato la Taifa
Na Damas Makangale, MOblog
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini nchini (Tanzania
Chamber of Minerals and Energy) Joseph Kahama amesema chama kwa
kushirikiana na chuo cha Ufundi Veta Moshi wataendelea kupeleka vijana
wazawa wa kitanzania kwenda kupata mafunzo ya mambo ya uchimbaji na
utafutaji wa Madini (Geology).
Akizungumza na MOblog jana kwenye mahojiano maalum baada ya kumaliza
mkutano wao wa mwaka kwa wanachama wake, Joseph Kahama amesema chama
chao kwa kushirikiana na serikali wataendelea kusaidia vijana wa
kitanzania kupata elimu ya kutosha katika sekta ya madini nchini.
“tumeshapeleka vijana kadhaa kwenye mafunzo mahsusi ya madini na
wengi wao wameshapata kazi katika kampuni kadhaa za madini hapa
Tanzania,” amesema.
Bw. Maswi akitoa neno na ahadi za serikali kuendelea kushirikiana wadau katika sekta ya madini nchini.
Mwenyekiti wa Tanzania Chamber of Minerals and Energy, Joseph
Kahama akizungumza wakati wa sherehe hizo jana usiki katika hoteli ya
Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Kahama alisisitiza kwamba si kweli kwa wageni wengi ndio
wameajiriwa katika sekta madini kuliko wazawa kwa sababu kwa takwimu
asilimia 90 walioajiriwa sasa katika migoi mbalimbali ni watanzania.
Alisisitiza kwamba wataendelea na mkakati wao wa kuwajengea uwezo
wa sawa (skills)katika uchimbaji na utafutaji wa madini ili kuongeza
ajira kwa vijana na kutokomeza umaskini hapa nchini.
Amesema kwa sasa wana malengo kwa kushirikiana na serikali
kuangalia kwa jinsi gani wanasema kuongeza mchango wa sekta ya madini
katika pato la taifa kutoka 3.7 asilimia mpaka asilimia 10.
Kahama amesema kwamba kwa kushirikiana na serikali wataendelea
kusukuma gurudumu la maendeleo kupitia sekta ya madini na kuhakikisha
kwamba wazawa wananufaika vya kutosha kutokana na mchango wa sekta hiyo
kwenye uchumi wa taifa.
Amesema pia wadau katika sekta hiyo wanawakaribisha wachimbaji
wadogo wadogo wawe wanachama wa chama chao ili waweze kusaidiana na
kukabiliana na changmoto mbalimbali.
Kahama aliahidi kwamba wanachama na wachimbaji wote wa madini
watashirikiana katika kuweka mazingira safi wakati wote wa utafutaji na
uchimbaji wa madini katika maeneo husika.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo Mabalozi wakifuatilia tukio hilo.
Wadau wa sekta ya madini nchini wakibadilishana mawazo kwenye Gala Dinner party ya wadau wa Sekta ya madini na Serikali iliyofanyika kwenye Golden Tulip jijini Dar.
Mgeni Rasmi katika sherehe za mwaka za Chama cha Wafanyabiashara
wa Madini Tanzania (Tanzania Chamber of Minerals and Energy) Katibu Mkuu
Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi akiongozana na Mwenyekiti
wa Tanzania Chamber of Minerals and Energy, Joseph Kahama kwenye meza
ya chakula wakati wa halfa ya chakula cha usiku iliyoandaliwa na Chama
cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na Mwenyekiti wa
Tanzania Chamber of Minerals and Energy wakiongoza wageni waalikwa
kupakua chakula.
Wageni waalikwa wakijisevia chakula cha usiku.
Mwenyekiti wa Tanzania Chamber of Minerals and Energy, Joseph Kahama akibadilishana mawazo na wageni waalikwa.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi akisalimiana na Mkurugenzi
Mtendaji wa Makampuni ya Ryan Bert and Compay Limited na Swordfish
Security Consultants Haki Ngowi liyeambatana na mdogo wake Mbunifu wa
mavazi nchini Sheria Ngowi.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi akifurahi jambo na baadhi ya wageni waalikwa.
Mwenyekiti wa Tanzania Chamber of Minerals and Energy, Joseph
Kahama akibadilishana mawazo na baadhi ya wadau wa sekta ya madini.
Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi na Wa pili kushoto Katibu Mkuu wa Tanzania Chamber of Minerals and Energy, Bw Emmanuel Jengo.
Makamu wa rais wa Africa Barrick Gold Bw. Deo Mwanyika (wa pili
kushoto) akibadilishana mawazo na Waheshimiwa mabalozi kwenye Gala
Dinner Party iliyoandaliwa na Tanzania Chamber of Minerals and Energy
kwenye hoteli ya Golden Tulip.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Eliakim Maswi akiteta jambo na Mmoja wa wadau katika sekta ya Madini.
Comments
Post a Comment