JAJI WARIOBA: KATIBA YA TANGANYIKA INAWEZA KUPATIKANA KWA MIEZI MITATU.

JAJI WARIOBA: KATIBA YA TANGANYIKA INAWEZA KUPATIKANA KWA MIEZI MITATU.

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akizungumza katika mkutano wake na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Dar es Salaam jana. 
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema Katiba ya Tanganyika inaweza kuandikwa ndani ya miezi mitatu tu kwa kuwa maoni mengi yaliyomo katika Rasimu ya Katiba iliyozinduliwa Jumatatu, kwa kiwango kikubwa yametoka kwa wananchi wa upande huo wa Muungano
Warioba alisema hayo jana wakati akizungumza na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), kwenye Ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam.
“Kutunga Katiba ya Tanganyika siyo kazi ngumu, ukisoma rasimu hii sura ya kwanza mpaka ya tano, sioni kama Katiba ya Tanganyika itakuwa tofauti na maoni yaliyomo katika sura hizo,” alisema na kuongeza:
“Misingi iliyopo katika utangulizi wa rasimu hii imetokana na maoni ya wananchi hao. Wakati wa kukusanya maoni, Zanzibar walijikita zaidi kwenye Muungano, maoni mengine kwa kiwango kikubwa yametoka kwa Watanzania Bara na katika kuandika Katiba ya Tanganyika sioni kama watabadilisha chochote kuhusu misingi hii ambayo ni; tunu za taifa, maadili, malengo na haki za binadamu.”
Alisema kuhusu kubadilishwa kwa mihimili ya Serikali na vyombo vingine vya kitaifa, kikubwa kinachoweza kuguswa ni muundo wa Bunge la Tanganyika, Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Baraza la Mawaziri.
“Kuhusu taratibu za kufanya kazi; iwe ni madaraka ya Rais, utaratibu wa kufanya kazi katika Bunge, Mahakama na Serikali sioni kama litakuja suala jipya kwa sababu mambo hayo yameshatolewa maoni. “Kilichobaki ni madaraka kwa umma tu, kwa maana ya Local Government (Serikali za Mitaa). Hata hili la madaraka kwa umma watakaolishughulikia watumie taarifa za wananchi waliotoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya. Wananchi walitoa maoni kuhusu jambo hili ambayo yapo wazi kabisa.”
Uchaguzi Mkuu 2015
Kuhusu uwezekano wa Katiba Mpya kutumika katika Uchaguzi Mkuu 2015, Jaji Warioba alisema Tume hiyo ilipewa muda mfupi wa kuandaa Rasimu ya Katiba kwa sababu ilielezwa kuwa uchaguzi wa mwaka 2015, utafanyika kwa kutumia Katiba Mpya.
“Katiba hii ilitakiwa iwe imekamilika Aprili mwaka huu, maana yake tungekuwa na mwaka mmoja na nusu wa kufanya mambo mengine ya kuwezesha itumike kwenye uchaguzi wa mwaka 2015,” alisema.
Alisema ndiyo maana katika rasimu hiyo, Tume imeweka masharti ya mpito ya miaka minne, kuanzia siku inapopatikana Katiba Mpya hadi Desemba 28, 2018.
Alisema rasimu hiyo imefafanua Baraza la Mawaziri na Bunge vitakuwaje… “Sasa hivi tuna Serikali na Bunge. Katiba Mpya itapatikana mwaka huu, lakini Bunge letu litaendelea kuwapo kwa msingi wa Katiba ya sasa mpaka ufike wakati wa uchaguzi, hiyo inafanyika kwa ajili ya kulinda uongozi wa Bunge na Serikali.”
Alisema ili kuwepo na Uchaguzi Mkuu kwa Katiba Mpya ni lazima itungwe Katiba ya Tanganyika, kwamba wamependekeza miaka minne ya mpito ili kutoa nafasi ya kubadilishwa kwa mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuundwa upya Tume ya Uchaguzi itakayoendesha uchaguzi kwa msingi wa Katiba Mpya.

“Siyo lazima kila kitu kikamilike baada ya miaka minne, kuna mambo yanaweza kubadilishwa kwa miezi sita au mwaka mmoja. Kila tulipobadili Katiba tulifanya jambo hili.
“Mfano ni mwaka 1984 tulipofanya mabadiliko makubwa ya Katiba ambayo ilileta ukomo wa Rais, haki za binadamu, waziri mkuu na mambo mengine makubwa. Kipindi hicho ilitungwa sheria mpya ya uchaguzi ambayo inatumika hadi sasa.”
Gharama Serikali tatu
Kuhusu hoja kwamba muundo wa Serikali tatu ni gharama, Jaji Warioba alisema hautakuwa na gharama kubwa kama inavyotafsiriwa na watu wengi.
Alisema kwa kulitambua hilo, ndiyo maana Tume ilipunguza ukubwa wa Serikali, ikiwa ni pamoja na kupendekeza idadi ya wabunge 75 na mawaziri wasiozidi 15.
“Hata uwepo wa Serikali mbili bado hautaweza kupunguza gharama. Katika hili ni muhimu kukubaliana na mawazo ya wananchi juu ya muundo wa Serikali tatu ambazo zimepunguza gharama. Tumependekeza Serikali ya Muungano kuwa na chanzo chake cha mapato ambayo ni ushuru wa bidhaa, mapato yasiyo ya kodi, michango kutoka nchi wahisani, mikopo na mapato mengine.”
“Wapo watu wanataka kugawa mikoa, wapo wanaopendekeza Jiji la Mbeya ligawanywe, wapo wanaotaka Songea igawanywe, hizi zote ni gharama… Sasa iweje kugawa mikoa isiwe gharama, Serikali tatu iwe na gharama? Hata kijiji ninachotoka zamani kilikuwa kimoja, sasa vimegawanywa vipo vitatu!”
Alisema Tanganyika ilipopata uhuru kulikuwa na majimbo manane tu, lakini sasa ipo mikoa 25 na wilaya, tarafa na vijiji zimegawanywa.
Alisema gharama za Serikali ya Muungano zitakuwa katika Wizara ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mambo ya Nje, taasisi ambazo tayari zipo, “Inashangaza kuona watu wakisema kuwa Tume kupendekeza Serikali tatu ni kwenda kinyume na mawazo ya Mwalimu Julius Nyerere.”
Kumsaliti Nyerere
Alisema hata Mwalimu Nyerere hakuwa na mawazo mgando. Alikuwa anatambua mabadiliko na mara kadhaa alibadilika kulingana na mahitaji ya wananchi na wakati.
Alitoa mfano akisema Mwalimu Nyerere alikuwa muumini wa mfumo wa chama kimoja, lakini mwaka 1992 baada ya Ripoti ya Jaji Francis Nyalali, alibadili mawazo na kuukubali mfumo huo licha ya asilimia 80 ya Watanzania kuupinga.

Alisema: “Maoni ya msingi yaliyomo katika rasimu hii yametokana na maoni ya wananchi, lakini vyombo vya habari vimejikita kuzungumzia mambo yanayohusu uongozi, hasa mambo ya kisiasa,” alisema Warioba huku akisisitiza kuwa Katiba hiyo siyo mali ya Tume wala kundi fulani katika jamii.
Alisema wananchi wamezungumzia matatizo ya kilimo, usafiri, afya, hifadhi ya jamii, maadili katika taifa na haki za binadamu… “Mambo haya katika kutoa habari hayakupewa kipaumbele, lakini mambo kuhusu kugombea urais, ubunge yalipewa kipaumbele kikubwa.”
Ukomo na uraia
Alisema tume hiyo inafanya kazi yake kwa kufuata sheria ya Mabadiliko ya Katiba na kwamba itamaliza muda wake itakapowasilisha rasimu hiyo katika Bunge Maalumu la Katiba.
Kuhusu uraia wa nchi mbili alisema: “Tulipopendekeza suala hili tulikuwa na maana kuwa isiwe lazima Mtanzania akipata uraia wa nchi nyingine awe amepoteza hadhi yake. Ndiyo maana tukasema katika rasimu kuwa atakuwa na hadhi maalumu.”
Alisema nchi nyingi duniani hutoa uraia kwa watu kutoka mataifa mbalimbali lakini hawawezi kugombea urais, kuingia katika jeshi la nchi husika, kwamba sheria lazima ifafanue juu ya Mtanzania kutopoteza haki zake za msingi.
{ Read More }


DK. SLAA - SERIKALI IKOMESHE "UKABURU" KWA RAIA


‘SERIKALI YA KIKWETE IKOMESHE ‘UKABURU’ DHIDI YA WATANZANIA’

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibroad Slaa amehitimisha ziara yake ya siku 22 ya kuimarisha na kukagua uhai wa chama katika majimbo 19 mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Singida, akiitaka Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha manyanyaso na ukatili wanaofanyiwa wananchi.

Amesema kuwa baada ya kuzungumza na wananchi hususan maeneo ya vijijini ambako alijikita kwa siku hizo 22, ameendelea kuthibitisha kuwa sehemu kubwa ya kero zinazowakabili Watanzania, hazihitaji gharama yoyote kuzimaliza ili wananchi waishi kwa amani katika nchi yao, akitolea mfano wa kero ya manyanyaso mbalimbali, hususan kutoka kwa vyombo vya dola. 

Amesisitiza kuwa kama Serikali ya Rais Kikwete inataka kupata uhalali mbele ya Watanzania na iwapo Rais mwenyewe anataka kumaliza muda wake na kuacha kumbukumbu kwa wananchi, inatakiwa kukomesha mara moja manyanyaso wanayofanyiwa wananchi, kwani kufanya hivyo ni wajibu wa serikali na hakuna gharama yoyote.


Akitolea mifano ya matukio ya kikatili na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa vyombo vya serikali kupitia matukio mbalimbali zikiwemo operesheni mbili za hivi karibuni, Tokomeza Ujangili na Kimbunga, Katibu Mkuu amesema kwa namna ambavyo serikali iliyoko madarakani inawatenda raia wake, Tanzania inavunja rekodi hata ya Afrika Kusini ya enzi za Makaburu.

“Tunamtaka Rais Kikwete kuacha kufanya kama afanyavyo baba asiyejali au baba wa kambo anayechukia watoto…JK ukitaka ubaki na heshima baada ya kuondoka madarakani, fanyia kazi orodha ya manyanyaso wanayofanyiwa wananchi. Tena mengi yanafanywa na polisi, jeshi na wakuu wa wilaya, watendaji wa vijiji na watendaji wa kata na madiwani.

“Yapo mengine ya kubambikia kesi watu, kunyang’anywa ardhi, kunyimwa haki kwa nuguvu tu, kuchangishwa michango haramu inayoambatana na vipigo na kunyang’anya watu mali zao, huku mapato na matumizi hayasomwi na kero nyingine kubwa ni migogoro ya ardhi. Kuachia manyanyaso haya dhidi ya wananchi ni kuonesha udhaifu mkubwa wa kiuongozi. Labda watuambie kuwa serikali hii ya CCM sasa imeshaamua kuwageuka raia wake. 

“Hauhitaji hata senti moja kuondoa manyanyaso ya serikali kupitia vyombo vya dola wanayofanyiwa wananchi. Mnapomtesa Mtanzania namna hii…watu wanateswa sana na kubambikiwa kesi, wanapigiliwa spoke sehemu za siri, wanawekewa chupa na kubakwa, mnataka aende kuishi wapi. 

“Hayo maendeleo mnayoyazungumza ni kwa ajili ya nani kama wananchi wanapigwa, kuteswa na kuuwawa bila hatia. Tumefikia mahali serikali inawatenda raia wake kuliko hata Makaburu walivyomtesa Mzee wetu Hayati Mandela alipokuwa gerezani. 

“Mwalimu Nyerere alisema ukaburu si rangi. Huu unaofanyika ni ukaburu ambao wakati ule wa ubaguzi wa rangi tuliimba sana shuleni na majeshini kupinga ukatili wa makaburu wa Afrika Kusini dhidi ya weusi waliokuwa wengi. Leo Serikali hii inafanyia raia wake matendo zaidi ya yale. Tunakwenda wapi. Kikwete chukua hatua.” 


“Kila nilikopita ni vilio vya manyanyaso, kuanzia Kakonko kule Wilaya ya Buyungu, kote huko Kasulu Vijijini viongozi wangu wote wa serikali nzima ya kijiji wamebambikwa kesi ya mauaji, wote kabisa. Hapo Nzega nimeshuhudia kwa macho yangu mateso wanayoyapata wachimbaji wadogo wadogo, wengine wamepigwa vibaya na askari polisi, tena machimbo yao yametekwa na viongozi wa wilaya na kuyageuza mali zao na sasa wanachuma pesa kwa kupiga raia.”

Katibu Mkuu Dkt. Slaa ambaye alianza ziara yake Desemba 4, mwaka huu kwa kufanya mkutano wa hadhara na kikao cha ndani Jimbo la Kahama, mkoani Shinyanga, amehitimisha ziara yake Desemba 23, kwa kuhutubia wananchi wa Vijiji vya Shelui na Nyengege, Jimbo la Iramba Magharibi.

Amewataka wanaCHADEMA kuuchukulia mchakato na mjadala wa Katiba Mpya ya Watanzania kuwa agenda ya muhimu, ya kudumu na lazima katika mikutano yao yote, ikiwemo ya ndani ya chama, hadhara au ‘vijiweni’, lengo la msingi liwe kuwataarifu wanachama na wananchi kwa ujumla, tulikotoka, tulipo na tunakokwenda. 

Ametumia ziara hiyo kuwasisitiza viongozi na wanachama wa CHADEMA nchi nzima kuhakikisha wanatekeleza maagizo mbalimbali ya vikao ya chama, hususan kwa sasa wasimamie kikamilifu maelekezo ya Waraka Katibu Mkuu Namba 6 wa mwaka 2013.

Waraka huo ambao unahusu mkakati wa kusukuma ujenzi wa misingi/matawi na uchaguzi wa ndani ya chama 2013/2014, umeelekeza viongozi nchi nzima namna ya kuendesha programu ya ‘M4C-CHADEMA ni Msingi’ inayoendelea nchi nzima, ikisimamiwa na kanda 10 za chama ambapo moja ya malengo mahsusi ni kusimika na kuimarisha chama kwenye vitongoji na mitaa.


“Ni lazima kila mwanaCHADEMA, wapenzi wa chama hiki, wananchi wenye mapenzi mema na ukombozi wa pili wa taifa lao, tuungane, tushikamane pamoja kusukuma jitihada hizi za kusimika chama chenu, ambacho ndiyo tumaini jipya la Watanzania katika ngazi ya chini kabisa ya uongozi katika nchi yetu.

“Viongozi wote wenye mapenzi mema na CHADEMA, kuanzia ngazi ya taifa hadi chini kabisa lazima wahakikishe CHADEMA ni msingi inakamilika kama ilivyokusudiwa,” amesisitiza Katibu Mkuu Dkt. Slaa katika ziara hiyo.

Katika kuwakumbusha juu ya waraka huo, Katibu Mkuu Dkt. Slaa amewasisitiza wanachama na viongozi umuhimu wa kuzingatia;

1. Kupata viongozi imara wa chama kuanzia ngazi ya chini kabisa ya msingi

2. Ratiba ya utekelezaji wa mkakati wa CHADEMA ni Msingi.

3. Ratiba ya uchaguzi wa ndani ya chama ngazi ya jimbo hadi taifa (pamoja na mabaraza ya chama), baada ya ngazi za chini kumalizika.

4. Kuzingatia taratibu za kikatiba za uchaguzi, kwani uchaguzi wa ‘mezani’ hautakubalika ndani ya CHADEMA.

5. Rushwa na kampeni chafu (katika uchaguzi kwa ngazi yoyote ile) hazitavumiliwa hata kidogo.

6. Maadili ya chama yasimamiwe kwa kila ngazi ya uchaguzi.

7. Ulinzi wa chama/ viongozi na wanachama ngazi zote, ambapo Red Brigade na BAVICHA ndiyo 
nguzo ya ulinzi.


Ukombozi wa kweli kwa mwananchi uanzie serikali za mitaa


Katibu Mkuu amewataka Watanzania kuelewa kuwa ukombozi wa kweli wa mwananchi utapatikana iwapo watu wataweza kuchagua viongozi imara, makini, waadilifu na wapenda watu kuanzia ngazi ya kitongoji, mtaa na kijiji na hatimaye madiwani ambao huunda halmashauri ya wilaya, mji, manispaa au jiji.


“Ikulu ya kwanza ya mwananchi ni hapa ulipo, hapa kijijini au mtaani kwako. Ikulu ya pili ni halmashauri yenu ya wilaya. Hizi ni sehemu muhimu sana katika kuhakikisha watu wetu wanapata matumaini, haki na hatimaye ustawi wa maendeleo ndani ya nchi yao. Hakuna maana yoyote kuichagua CHADEMA iende Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam halafu huku mnaweka watu wabovu. Itakuwa sawa na kazi bure,”amesisitiza Katibu Mkuu Dkt. Slaa.

Amesema kuwa hasa wakati huu ambapo Taifa linajiandaa kwenda kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014, Watanzania wanapaswa kutambua umuhimu wa halmashauri za serikali za mitaa katika kusukuma maendeleo ya watu katika maeneo yao wanayoishi.

Amesisitiza kuwa katika ngazi hiyo ya uongozi, si kazi ngumu kumtambua mtu ambaye anaweza kuwa kiongozi mwadilifu, makini mwenye uwezo na mpenda watu, kwa sababu watu wote wanafahamiana kutokana na kuishi pamoja.

Pinda kubanwa chaguzi serikali za mitaa
“Katika ziara yangu hii ya siku 22, nimebaini kuwa kuna maeneo mengi sana ya vijiji ama hayana serikali kabisa, sehemu nyingine mwenyekiti hayupo au wajumbe, lakini Serikali ya CCM kupitia kwa wakurugenzi inaogopa kuitisha uchaguzi, kisa wanaogopa wakiitisha uchaguzi CHADEMA itashinda.

“Sasa napenda kutumia mkutano wangu huu wa kuhitimisha ziara hii, kutoa maagizo kwa viongozi wa chama wilaya na majimbo, kutuandikia taarifa ya kina Makao Makuu, ikieleza maeneo yote ya serikali za mitaa ambayo yako wazi na wakurugenzi hawajatangaza au hawataki kutangaza ndani ya muda unaotakiwa kisheria uchaguzi wa kuziba nafasi kufanyika.

“Tunataka taarifa za kina ambazo tutazitumia kumbana Mizengo Pinda maana yeye ndiye anahusika kusimamia Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa au TAMISEMI. Hatuwezi kukubali kuona wananchi wanakosa haki yao ya uwakilishi kwa sababu tu CCM wanaogopa ukiitishwa uchaguzi CHADEMA tutashinda. Katika hili pia tutakufa na Pinda,” amesema Katibu Mkuu.

Katibu Mkuu Dkt. Slaa ametembelea jumla ya majimbo 19 ambayo ni; Kahama (Shinyanga), Kakonko, Muhambwe, Kasulu Vijijini, Kasulu Mjini, Buhigwe, Kigoma Kaskazini, Kigoma Mjini, Kigoma Kusini; mkoani Kigoma. Mengine ni;

Kaliua, Urambo, Tabora Kaskazini, Tabora mjini, Sikonge, Igalula, Bukene, Nzega, Igunga (Tabora) na Iramba Magharibi mkoani Singida.

Katika maeneo yote aliyotembelea, Katibu Mkuu Dkt. Slaa amepokea kero na ushauri wa wanachama na Watanzania kwa ujumla, kuhusu masuala mbalimbali ya chama na nchi, ya kitaifa na mengine yanayohusu maeneo husika (local politics), kwa njia kadhaa ikiwemo taarifa za viongozi kuhusu utendaji wa chama, kupitia maswali na maoni katika mikutano pamoja na kufika mwenyewe kujionea hali halisi ya baadhi ya masuala aliyoambiwa.
‘SERIKALI YA KIKWETE IKOMESHE ‘UKABURU’ DHIDI YA WATANZANIA’

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibroad Slaa amehitimisha ziara yake ya siku 22 ya kuimarisha na kukagua uhai wa chama katika majimbo 19 mikoa ya Shinyanga, Kigoma, Tabora na Singida, akiitaka Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukomesha manyanyaso na ukatili wanaofanyiwa wananchi.

Amesema kuwa baada ya kuzungumza na wananchi hususan maeneo ya vijijini ambako alijikita kwa siku hizo 22, ameendelea kuthibitisha kuwa sehemu kubwa ya kero zinazowakabili Watanzania, hazihitaji gharama yoyote kuzimaliza ili wananchi waishi kwa amani katika nchi yao, akitolea mfano wa kero ya manyanyaso mbalimbali, hususan kutoka kwa vyombo vya dola. 

Amesisitiza kuwa kama Serikali ya Rais Kikwete inataka kupata uhalali mbele ya Watanzania na iwapo Rais mwenyewe anataka kumaliza muda wake na kuacha kumbukumbu kwa wananchi, inatakiwa kukomesha mara moja manyanyaso wanayofanyiwa wananchi, kwani kufanya hivyo ni wajibu wa serikali na hakuna gharama yoyote.


Akitolea mifano ya matukio ya kikatili na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa vyombo vya serikali kupitia matukio mbalimbali zikiwemo operesheni mbili za hivi karibuni, Tokomeza Ujangili na Kimbunga, Katibu Mkuu amesema kwa namna ambavyo serikali iliyoko madarakani inawatenda raia wake, Tanzania inavunja rekodi hata ya Afrika Kusini ya enzi za Makaburu.

“Tunamtaka Rais Kikwete kuacha kufanya kama afanyavyo baba asiyejali au baba wa kambo anayechukia watoto…JK ukitaka ubaki na heshima baada ya kuondoka madarakani, fanyia kazi orodha ya manyanyaso wanayofanyiwa wananchi. Tena mengi yanafanywa na polisi, jeshi na wakuu wa wilaya, watendaji wa vijiji na watendaji wa kata na madiwani.

“Yapo mengine ya kubambikia kesi watu, kunyang’anywa ardhi, kunyimwa haki kwa nuguvu tu, kuchangishwa michango haramu inayoambatana na vipigo na kunyang’anya watu mali zao, huku mapato na matumizi hayasomwi na kero nyingine kubwa ni migogoro ya ardhi. Kuachia manyanyaso haya dhidi ya wananchi ni kuonesha udhaifu mkubwa wa kiuongozi. Labda watuambie kuwa serikali hii ya CCM sasa imeshaamua kuwageuka raia wake. 

“Hauhitaji hata senti moja kuondoa manyanyaso ya serikali kupitia vyombo vya dola wanayofanyiwa wananchi. Mnapomtesa Mtanzania namna hii…watu wanateswa sana na kubambikiwa kesi, wanapigiliwa spoke sehemu za siri, wanawekewa chupa na kubakwa, mnataka aende kuishi wapi. 

“Hayo maendeleo mnayoyazungumza ni kwa ajili ya nani kama wananchi wanapigwa, kuteswa na kuuwawa bila hatia. Tumefikia mahali serikali inawatenda raia wake kuliko hata Makaburu walivyomtesa Mzee wetu Hayati Mandela alipokuwa gerezani. 

“Mwalimu Nyerere alisema ukaburu si rangi. Huu unaofanyika ni ukaburu ambao wakati ule wa ubaguzi wa rangi tuliimba sana shuleni na majeshini kupinga ukatili wa makaburu wa Afrika Kusini dhidi ya weusi waliokuwa wengi. Leo Serikali hii inafanyia raia wake matendo zaidi ya yale. Tunakwenda wapi. Kikwete chukua hatua.” 


“Kila nilikopita ni vilio vya manyanyaso, kuanzia Kakonko kule Wilaya ya Buyungu, kote huko Kasulu Vijijini viongozi wangu wote wa serikali nzima ya kijiji wamebambikwa kesi ya mauaji, wote kabisa. Hapo Nzega nimeshuhudia kwa macho yangu mateso wanayoyapata wachimbaji wadogo wadogo, wengine wamepigwa vibaya na askari polisi, tena machimbo yao yametekwa na viongozi wa wilaya na kuyageuza mali zao na sasa wanachuma pesa kwa kupiga raia.”

Katibu Mkuu Dkt. Slaa ambaye alianza ziara yake Desemba 4, mwaka huu kwa kufanya mkutano wa hadhara na kikao cha ndani Jimbo la Kahama, mkoani Shinyanga, amehitimisha ziara yake Desemba 23, kwa kuhutubia wananchi wa Vijiji vya Shelui na Nyengege, Jimbo la Iramba Magharibi.

Amewataka wanaCHADEMA kuuchukulia mchakato na mjadala wa Katiba Mpya ya Watanzania kuwa agenda ya muhimu, ya kudumu na lazima katika mikutano yao yote, ikiwemo ya ndani ya chama, hadhara au ‘vijiweni’, lengo la msingi liwe kuwataarifu wanachama na wananchi kwa ujumla, tulikotoka, tulipo na tunakokwenda. 

Ametumia ziara hiyo kuwasisitiza viongozi na wanachama wa CHADEMA nchi nzima kuhakikisha wanatekeleza maagizo mbalimbali ya vikao ya chama, hususan kwa sasa wasimamie kikamilifu maelekezo ya Waraka Katibu Mkuu Namba 6 wa mwaka 2013.

Waraka huo ambao unahusu mkakati wa kusukuma ujenzi wa misingi/matawi na uchaguzi wa ndani ya chama 2013/2014, umeelekeza viongozi nchi nzima namna ya kuendesha programu ya ‘M4C-CHADEMA ni Msingi’ inayoendelea nchi nzima, ikisimamiwa na kanda 10 za chama ambapo moja ya malengo mahsusi ni kusimika na kuimarisha chama kwenye vitongoji na mitaa.


“Ni lazima kila mwanaCHADEMA, wapenzi wa chama hiki, wananchi wenye mapenzi mema na ukombozi wa pili wa taifa lao, tuungane, tushikamane pamoja kusukuma jitihada hizi za kusimika chama chenu, ambacho ndiyo tumaini jipya la Watanzania katika ngazi ya chini kabisa ya uongozi katika nchi yetu.

“Viongozi wote wenye mapenzi mema na CHADEMA, kuanzia ngazi ya taifa hadi chini kabisa lazima wahakikishe CHADEMA ni msingi inakamilika kama ilivyokusudiwa,” amesisitiza Katibu Mkuu Dkt. Slaa katika ziara hiyo.

Katika kuwakumbusha juu ya waraka huo, Katibu Mkuu Dkt. Slaa amewasisitiza wanachama na viongozi umuhimu wa kuzingatia;

1. Kupata viongozi imara wa chama kuanzia ngazi ya chini kabisa ya msingi

2. Ratiba ya utekelezaji wa mkakati wa CHADEMA ni Msingi.

3. Ratiba ya uchaguzi wa ndani ya chama ngazi ya jimbo hadi taifa (pamoja na mabaraza ya chama), baada ya ngazi za chini kumalizika.

4. Kuzingatia taratibu za kikatiba za uchaguzi, kwani uchaguzi wa ‘mezani’ hautakubalika ndani ya CHADEMA.

5. Rushwa na kampeni chafu (katika uchaguzi kwa ngazi yoyote ile) hazitavumiliwa hata kidogo.

6. Maadili ya chama yasimamiwe kwa kila ngazi ya uchaguzi.

7. Ulinzi wa chama/ viongozi na wanachama ngazi zote, ambapo Red Brigade na BAVICHA ndiyo 
nguzo ya ulinzi.


Ukombozi wa kweli kwa mwananchi uanzie serikali za mitaa


Katibu Mkuu amewataka Watanzania kuelewa kuwa ukombozi wa kweli wa mwananchi utapatikana iwapo watu wataweza kuchagua viongozi imara, makini, waadilifu na wapenda watu kuanzia ngazi ya kitongoji, mtaa na kijiji na hatimaye madiwani ambao huunda halmashauri ya wilaya, mji, manispaa au jiji.


“Ikulu ya kwanza ya mwananchi ni hapa ulipo, hapa kijijini au mtaani kwako. Ikulu ya pili ni halmashauri yenu ya wilaya. Hizi ni sehemu muhimu sana katika kuhakikisha watu wetu wanapata matumaini, haki na hatimaye ustawi wa maendeleo ndani ya nchi yao. Hakuna maana yoyote kuichagua CHADEMA iende Ikulu ya Magogoni, Dar es Salaam halafu huku mnaweka watu wabovu. Itakuwa sawa na kazi bure,”amesisitiza Katibu Mkuu Dkt. Slaa.

Amesema kuwa hasa wakati huu ambapo Taifa linajiandaa kwenda kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2014, Watanzania wanapaswa kutambua umuhimu wa halmashauri za serikali za mitaa katika kusukuma maendeleo ya watu katika maeneo yao wanayoishi.

Amesisitiza kuwa katika ngazi hiyo ya uongozi, si kazi ngumu kumtambua mtu ambaye anaweza kuwa kiongozi mwadilifu, makini mwenye uwezo na mpenda watu, kwa sababu watu wote wanafahamiana kutokana na kuishi pamoja.

Pinda kubanwa chaguzi serikali za mitaa
“Katika ziara yangu hii ya siku 22, nimebaini kuwa kuna maeneo mengi sana ya vijiji ama hayana serikali kabisa, sehemu nyingine mwenyekiti hayupo au wajumbe, lakini Serikali ya CCM kupitia kwa wakurugenzi inaogopa kuitisha uchaguzi, kisa wanaogopa wakiitisha uchaguzi CHADEMA itashinda.

“Sasa napenda kutumia mkutano wangu huu wa kuhitimisha ziara hii, kutoa maagizo kwa viongozi wa chama wilaya na majimbo, kutuandikia taarifa ya kina Makao Makuu, ikieleza maeneo yote ya serikali za mitaa ambayo yako wazi na wakurugenzi hawajatangaza au hawataki kutangaza ndani ya muda unaotakiwa kisheria uchaguzi wa kuziba nafasi kufanyika.

“Tunataka taarifa za kina ambazo tutazitumia kumbana Mizengo Pinda maana yeye ndiye anahusika kusimamia Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa au TAMISEMI. Hatuwezi kukubali kuona wananchi wanakosa haki yao ya uwakilishi kwa sababu tu CCM wanaogopa ukiitishwa uchaguzi CHADEMA tutashinda. Katika hili pia tutakufa na Pinda,” amesema Katibu Mkuu.

Katibu Mkuu Dkt. Slaa ametembelea jumla ya majimbo 19 ambayo ni; Kahama (Shinyanga), Kakonko, Muhambwe, Kasulu Vijijini, Kasulu Mjini, Buhigwe, Kigoma Kaskazini, Kigoma Mjini, Kigoma Kusini; mkoani Kigoma. Mengine ni;

Kaliua, Urambo, Tabora Kaskazini, Tabora mjini, Sikonge, Igalula, Bukene, Nzega, Igunga (Tabora) na Iramba Magharibi mkoani Singida.

Katika maeneo yote aliyotembelea, Katibu Mkuu Dkt. Slaa amepokea kero na ushauri wa wanachama na Watanzania kwa ujumla, kuhusu masuala mbalimbali ya chama na nchi, ya kitaifa na mengine yanayohusu maeneo husika (local politics), kwa njia kadhaa ikiwemo taarifa za viongozi kuhusu utendaji wa chama, kupitia maswali na maoni katika mikutano pamoja na kufika mwenyewe kujionea hali halisi ya baadhi ya masuala aliyoambiwa.
 

Comments

Popular posts from this blog

alahh hii ni kali ya mwaka madam Martha!-3

ANGALIA PICHA ZA KANGA MOKO BALAA INYE NJE NJE!